KKKT USHARIKA WA KIJITONYAMA IBADA YA EVENING GLORY 19/06/2019
UJUMBE WA LEO:
"JINASUE NA MITEGO YA UOVU"
(CHAKULA NI IBADA)
( CHAKULA CHA KIPEPO )
1 Wakoritho 10 : 19 - 22
Isaya 28 :7 - 8
Daniel 1 : 5 - 8
Zaburi 141 : 4
Ezekiel 13 : 17
1 Wakoritho 10 : 19 - 22
19 Basi niseme nini? Ya kwamba kile kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu? Au ya kwamba sanamu ni kitu?
20 Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani.
21 Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani.
22 Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?
Isaya 28 :7 - 8
7 Lakini hawa nao wamekosa kwa divai, wamepotea kwa kileo; kuhani na nabii wamekosa kwa kileo, wamemezwa kwa divai, wamepotea kwa kileo; hukosa katika maono, hujikwaa katika hukumu.
8 Maana meza zote zimejaa matapiko na uchafu, hapana mahali palipo safi.
Daniel 1 : 5 - 8
5 Huyo mfalme akawaagizia posho ya chakula cha mfalme, na ya divai aliyokunywa, akaagiza walishwe hivyo muda wa miaka mitatu; ili kwamba hatimaye wasimame mbele ya mfalme.
6 Basi katika hao walikuwapo baadhi ya wana wa Yuda, Danieli, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria.
7 Mkuu wa matowashi akawapa majina; alimwita Danieli, Belteshaza; na Hanania akamwita Shadraka; na Mishaeli akamwita Meshaki; na Azaria akamwita Abednego.
8 Lakini Danieli aliazimu moyoni mwake ya kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme, wala kwa divai aliyokunywa; basi akamwomba yule mkuu wa matowashi ampe ruhusa asijitie unajisi.
Zaburi 141 : 4
4 Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya, Nisiyazoelee matendo yasiyofaa, Pamoja na watu watendao maovu; Wala nisile vyakula vyao vya anasa.
Ezekiel 13 : 17
17 Na wewe, mwanadamu, kaza uso wako juu ya binti za watu wako, watabirio kwa akili zao wenyewe; ukatabiri juu yao,
Mhubiri: Mwl. Eng. Tumainiel Mbwambo
Kwa maombi na ushauri :
Mch. Dkt. Eliona Kimaro.
Simu :+255655516053, +255754516053
YouTube : Rev. Dr. Eliona Kimaro TV
Barua Pepe:
[email protected]